Monday, August 1, 2011

Jay Z na Kanye kwenye album moja.......

 Nakubali kuwa mwanahip-pop Jay-Z anahusishwa na hili swala la mpinga kristo yaani Freemaso lakini bado siwezi kumhesabu nje ya waasisi wa mziki wa hip-pop na anayewika mpaka leo hii.
 Bado anazikamata hisia za mashabiki wengi duniani kwa kila nyimbo anayoachia kwenye industry hii ya muziki.
 Hivi karibuni akiwa na rapper ambaye na yeye anahusishwa na mambo ya Freemason hapa namzungumzia Kanye west, wametangaza tarehe rasmi watakayoingiza sokoni album yao mpya walioifanya pamoja.
 Marafiki hawa kwenye moja ya mahojiano walisema album hiyo iitwayo "The throne" itaingia sokoni tarehe 8 August, wamesema kuwa itaanza kuingia iTUNES na siku nne baadae yaani tarehe 12 August wasambazi wengine wataipoata pia album hiyo.
 Wamesisitiza mashabiki wao kuwa ndani ya album hiyo kutakuwa na mazuri zaidi ya wanchokisikia kwenye moja ya nyimbo ambayo wameshaitoa iitwayo "Otis" wakimshrikisha mkali wa RnB Otis Redding.
 Hivyo basi kwa wale mashabiki wa wanahip-pop hawa yani Jay na Kanye, tukae mkao wa kula mnamo tarehe nane ambayo kwa hapa TZ itakuwa sikukuu ya nananane tuingie iTunes na tununue album hiyo iliyosubiriwa kwa muda mrefu.
                                                                    Ian.

Amber asema na wanaopenda kupiga picha za.......!


 Kwenye dunia ya leo ni swala la kawaida rafiki, ndugu jamaa na zaidi zaid wapenzi kupigana picha ambazo kwa ukawaida zinakuwa kama hali ya kufurahia maisha yao au kwa ajili ya kumbukumbu muhimu.
 Hii huwa rahisi zaidi kutokana na uaminifu uliopo kati yako na mwenzako, sio hivyo tu hata kushare simu, laptops na mara nyingine unaweza kukuta watu ambao wako kwenye mahusiano wanapeana passwords za simu, emails na hata password za ATM ili panapotokea ulazima inakuwa rahisi kujikimu kifedha.
 Lakini mwanamitindo maarufu na mpenzi wa zamani wa rapa Kanye west swala la uaminifu kwa rafiki na watu wake wa karibu halikuzaa matunda na badala yake kuleta matatizo kwenye maisha yake mara baada ya watu aliyowaamini sana kusamabaza picha zake za siri kwenye mitandao bila idhini yake rasmi.
 Kwa kinywa chake mwanamitindo huyo alisema maneno makali na yenye mafunzo ndani yake ambayo ni salama kama rafiki utayapata pia.
 Amber alisema;
"I trusted someone who worked for me and allowed them to use my lap top millions times, i cought them sending my pics to themselves. I fired them immediately. Wiz and i and both our families knows have know abowt this for a month now.
 These pics are 2 and half years old, when i just sit in my computer am realy hurt, i have too many young girls who are looking up to me. I wouldnt have put these pics my self.
 The company that i was working with no longer wants me to work with them because of these pics and prevents me to get money to take care of my family. It is messed up situation when someone comes into ur life and and tries to destroy it.
 I know i am not the only girl in the world that has taken pics like that but they were very private.
 I am very sorry for letting my young rosebuds down, please understand that was result of trusting a person that didnt deserve my trust. I have cried for the past two two days but i know this too shall past, thank u all for ur support"
 Kuna mwenye swali, hope hakuna ila kama upo tuma kwenda email ya Bloglab enterprices, na utapata majibu.
                                         John Masunga Didas.

Nicki Minaj anmwiga Lil`mama kweli....????


 Ni juzi juzi tu mwanadada mkali wa hip pop duniani yaani Lil'mama alitanabaisha kuwa yeye ni Trendsetter, yaani kiongozi wa style ya nywele anayoitumia sana mwana hip pop mwenzake Nicki Minaj.
 Zaidi lil mama alisema kuwa Nicki Minaj alianza kutumia mtindo huo wa nywele mara tu baada ya kuhudhuria moja kati ya maonyesho ya lil mama lililoitwa Amarican best dance crew.
 Lil mama kwa msisitizo alisema sio tu mtindo huo wa nywele anaotumia Nicki Minaj, bali ni vitu vingi watu wanaiga kutoka kwake, mfano alisema style yake ya ukali kwenye kurap ambayo pia Nicki amekuwa akiitumia sana, pia aliongeza kwa kusema kuwa hata jinsi anavyovaa na jinsi anavyoandaa mziki wake watu huiga sana toka kwake.
 Ila rapper huyo ameeleza furaha yake kuona watu wengi wakiiga mambo yake na kueleza kuwa hiyo inaonyesha kuwa yeye ni mzuri sana ndo mana watu wengi wamekuwa wakimuiga.
                                                                                                            Masekepa Asangama.

Saturday, July 30, 2011

Man U mtalipa kisasi au mta........


 Mabingwa wa Champions League yaani Barcelona, wanayo shuguli nzito kwa kipindi mwisho wa mwezi wa saba na mwezi August barani America.
 Wakiwa bara la Amerika watakutana na timu tatu tofauti moja kati ya timu hizo ni mashetani wekundu yaani Man Utd.
 Ingawa Sir. Alex, kocha wa timu ya Man U bado hajaonyesha imani yake nakikosi chake lakini DeGae amesikika akijitapa na kuisifia timu yake kuwa anaamini itatoka na ushindi mkubwa kwenye mechi hiyo itakayo chezwa tarehe 31 mwezi huu.
 Wadau wa mpira wa miguu duniani akiwemo Pele, wanaufananisha mchezo huu kama vita vya malipizi maana ikumbukwe kuwa mnamo tarehe 28 mwezi Mei mwaka huu timu hizi zilikutana kwenye fainali za kombe la Champions League.
 Matokeo ya fainali ile yaliiacha dunia nzima ya mpira wa miguu midomo wazi baada ya Man U kupokea kichapo cha magoli 3-0, mmoja kati ya wakali walioiumiza Man U wengine hupenda kumuita DOKTA yaani Messi hatokuwepo kwenye kikosi cha Barca baada ya kuwa yupo kwenye likizo kwao Argentina.
 Barca watakuwa wakicheza 4-3-3, akiwemo Valles, Abidal, Pique, Puyol, Fontas, Thiago, Benquet, Iniesta, Afellay, Jonathan bila kumsahau Villa.
 Pia Man U itasukuma mtanange huu ikiwa inacheza 4-3-3, ikimchezesha De Gae, Vidic, Ferdinand, Evra, Young, Carrick,  Anderson, Park,Berbatov, Rooney.
 Barcelona pia wakiwa bado bara la Amerika watachuana na CD Gadalajara mnamo tarehe 3 August na Club America mnamo tarehe 6 August.
 Usiku wa kuamkia leo nahisi jiji letu litakuwa na shamsham sana, yaani tukimaliza tu shngwe za fiesta 2011, usiku mzito tutakuwa tanapagawa na mechi hii kati ya Man U na Barca pale Washington DC.
                                                                                                      Masekepa Asangama

Luda ana zaidi ya show na swagg "TUJIFUNZE"


 Mshkaji anaitwa Christopher Brian Bridges kwa jina kamili, nimejiuliza hii aka ya Ludcriss ilikujaje nakosa jibu sahii, maana haifanani kabisa na jina lake halisi....
 Jamaa alizaliwa mwaka 1977, Sep 11 pale Champaign nchini U.S.A...
 Alianza mziki 1998 na leo ana album saba na leo atakuwa na bonge moja la concert hapa jijini kwenye viwanja vya Leaders Club.
 Najua marafiki wengi tutakuwa pale usiku huu, ila kama rafiki nimewaokotea kastory nataka kushare na nyinyi kumhusu Luda.
 Kama nlivyokwisha sema kuwa hii ni album ya saba ya msanii huyu, inaitwa "Battle of sexes" ambayo aliiachia tarehe 9, march mwaka huu.
 Idea ya album hii ilikuwa kuwakutanisha Luda na mmoja kati ya wasanii walio chini ya lebo yake iitwayo "disturbing the peace au DTP". Yani kama unavyoona Lil'wayne alivyokuwa na Nicki Minaj kwenye album yao mpya.
 Mapema kabla ya kumaliza kurekodi album hiyo ambayo kabla yakupewa jina la battle of sexes ilipewa jina la back to back, mwanadada huyo kwa jina la Shawnna alivunja mkataba na lebo ya Luda na kuhamia kwenye lebo ya T-Pain iitwayo Nappy boy Ent.
 Kuhama kwa mwanadada huyo kulivuruga sana ratiba za Ludacriss na kupelekea kuanza upya kurekodi album hiyo na kuiita Batte of sexes.
 Licha ya tatizo hilo Luda alifanikiwa kumaliza kurekodi album hiyo na tarehe 8 Dec 2009 alichia ngoma ya kwanza kutoka kwenye album hiyo na nyimbo hiyo "how low" ilifanya vizuri na mwanzo wa mwaka huu aliachia album na ilifika mauzo ya Gold baada ya kuuza nakala 137000 kwa wiki ya kwanza sokoni.
 Swala linakuja Je! Ingekuwa ni msanii wa bongo falva kakutwa na matatizo kama hayo angemaliza kurekodi hiyo album kweli?
 Hakika HAPANA, zaidi wangeishia kulumabana kwenye vituo vya habari na kutupiana maneno tu mwisho kuharibu heshima zao na vipaji vyao pia,
                                                                                                            Africa Nyumbani.

Friday, July 29, 2011

Tusiharibu mimba, watoto ni faraja kubwa.....

 Jina langu ni "baba wawili", ni kijana wa kawaida kabisa na ili kuthibitisha ukawaida wangu jamani hata kazi maalum sina, ila hilo sio tatizo sana kwangu.
 Ishu ni hawa madogo wawili "mapacha" wangu, ambao niliwapata nikiwa mdogo sana.... Na hiyo ndio sababu leo timu ya bloglab imetoa nafasi hii kwangu ili niwe naandika kuhusu maisha yangu na watoto wangu ili kijana yeyote atakaye soma simulizi hizi apate nguvu kimaisha kuhusu familia na hatma yake namba ya vijana wanaotoa mimba kila siku na hata wanaopoteza maisha kupungua kabisa.
 Kama nlivyokwisha kusema kuwa niliwapata hawa mapacha nikiwa mdogo sana, na mara nyingi vijana kama mimi ambao wanakuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi mara tu linapotokea swala la mimba mahusiano hulegalega sana.
 Sawa hata mimi siwezi kukataa hata mara moja kuwa siku ile mama wawili aliponiambia kuwa anahisi ana ujauzito sikupata mshtuko, HAPANA! Nilipata mshtuko tena mkubwa sana, nakumbuka tulikuwa nyumbani kwangu, hata hamu ya kuendelea kupumzika iliisha na niliamua kuondoka zangu na kumwacha mpenzi wangu chumbani peke yake.
 Sawa sababu ni nyingi sana ambazo humpelekea kijana kupatwa mshtuko na hatma yake kuamua maamuzi hasi ili kuondokana na jambo hilo kabisa, wengine hukimbia mpaka miji ili kuepuka tatizo, wengine hukataa kabisa kuwa hawahusiki na ujauzito huo na wengine huthubutu kufanya "abortion" yaani kuitoa mimba.
 Ila nisingependa kuwa mwalimu kwa kiasi kikubwa bali kusimulia tu maisha yangu na wanangu hawa, ndani ya simulizi hizi pia kijana utapata mambo meengi mazuri na hii itakujenga hata siku utakapo kuwa na hali kama yangu iwe rahisi kuendanna na hali hiyo.
 Doto anaitwa "Dido" na kulwa "Obama", nawapenda sana..... Mara nyingine natamani wawe marafiki zangu na kuutoa huu ubaba kabisa labda wangenipenda zaidi na kuniamini bila kuwapo chembe ya uoga kuwa mi ni baba ntawachapa au ntawakasirikia...
 Naamini sio rahisi ila sitochoka kuwajengea imani hiyo ndo maana hata ukija nyumbani siku moja utasikia wananiita "kaka", na naamini ipo siku wataniita rafiki pia.
 Wameleta faraja kubwa kwenye familia yangu, faraja ambayo mimi na mama yao hatukuwa nayo kabla... Sasa ndani ni furaha tu, Dido atacheza hivi Obama vile basi ni furaha tupu jamani....
 Nakaaga na kuwaza je mimi na mama yake tungeamua kuitoa mimba, watoto hawa wangekuwa wapi leo.... Je! Furaha hii tungeipata wapi tena, hakika tusingeipata popote. Basi kumbe ulikuwa uamuzi wa busara sana kutokuikana mimba.
 Ingawa ulikuwa uamuzi mzito sana, kwani sikuwa na kazi, mama pia hakuwa na kazi.... Wapi tungepata pesa za kuwalisha watoto hawa? Kila jibu lililokuja wakati hule lilikuwa tatizo. Lakini tulipiga moyo konde na kuamua kuilea.
 Haya leo ngoja niishie hapa.... Ila jamani vijana wenzangu "mimba" msizitupe...... Mtoto huwa neema kubwa jamani, natamani mngeniona na furaha yangu leo.
                                                                                                         Tukutane wiki ijayo
                                                                                                                   Baba Wawili

Nicki Minaj na Roman Zolanski ni TWINS!!!!



 Licha ya umaarufu alionao Nicki Minaj, vituko na habari tofauti kumuhusu zinazaliwa kila kukicha.
 Hivi karibuni ametoa kali baada ya kumtambulisha dada yake ambaye ni pacha wake, Nicki Minaj akiwa kwenye moja ya mahojiano kwenye kituo maarufu cha matangazo kijulikanacho kama VIBE, alinukuliwa akisema "the one you see in buttoms up song with Trey, thats not Nicki Minaj, instead she is Roman Zolanski".
 Ina maana muda wote ulimwengu ukidhani kuwa yule ni Minaj, yeye mwenyewe alikana na kusema yule si yeye ni pacha wake Roman Zolanski.
 Pia alitanabaisha kuwa mama yao anasikika kwenye remix ya nyimbo ya romans revenge akirap sehemu ndogo kwa lafudhi ya kiingereza cha ya uingereza.
 Zaidi Minaj alisema "Roman was born inside me, i become her when i get ungry, she is a demon inside me".... Pia wanaharakati wa hip pop wamemfananisha Roman na Slim shady ambaye nayeye ni demon wa Eminems.
 Ndio sababu remix ya nyimbo ya Romans revenge, mwanadada Minaj aliamua kuwakutanisha wakali hawa yaani Roman Zolanski na Slim shady.
 Swala ni kwamba je kwa hapa TZ wapo wasanii wanaowajua ndugu zao kwa maana ya mizuka yao, na kuwatumia vizuri.... Au ni bangi tu mwanzo mwisho?
                                                                                           Baadae rafiki zangu,
                                                                                                                    Ian.